CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
Uongozi wa CCM Kata ya Mwananyamala Wilaya ya Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kushirikiana na uongozi wa CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar, wamempongeza kwa dhati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati, hasa mradi wa Treni ya SGR (Standard Gauge Railway), ambao umeleta suluhu kubwa kwa changamoto za usafiri wa nchi kavu nchini.
Pongezi hizo zimetolewa na viongozi na wanachama wa CCM kutoka Kata ya Mwananyamala na CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar walioshiriki katika ziara ya kutembelea mradi huo.
Ziara hiyo ilianza kwa kupanda treni kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, ambapo viongozi hao walielezea kutambua na kuthamini juhudi hizo za Serikali, wakikiri kuwa mradi wa SGR umeleta mabadiliko makubwa katika sekta ya usafiri nchini.
Akizungumza katika ziara hiyo, Katibu wa Siasa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar, Bi. Msekwa Mohamed Ali, alisema kuwa kupitia ziara hiyo wamejionea kazi kubwa na nzuri iliyofanywa katika mradi wa kimkakati wa SGR, akisisitiza kuwa mradi huo umeonyesha matumizi sahihi ya fedha za walipa kodi.
Aliwataka wananchi kumpongeza Rais Samia kwa juhudi hizo na kuendelea kumunga mkono kwa kusafiri na treni hiyo katika safari mbalimbali, ili wawe mashuhuda wa mafanikio hayo.
Naye Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mwananyamala, Pili Muongela, alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake kwa kutekeleza kwa ufanisi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, hasa mradi wa SGR, ambao umekuwa mwarobaini wa kumaliza tatizo la usafiri nchini.
Akitoa ufafanuzi wa ziara hiyo, Katibu wa CCM Kata ya Mwananyamala, Stanly Rufini Mvungi, alisema kuwa ziara hiyo pia ilihusisha kutembelea miradi mingine, ikiwemo sekta ya utalii kupitia Mradi wa Royal Tour, ambapo walifanya utalii wa ndani katika Hifadhi ya Mikumi, mkoani Morogoro, na kujionea wanyama pori na vivutio mbalimbali.
Alisisitiza kuwa ziara hiyo ni sehemu ya kuthamini mafanikio ya miradi mikubwa ya kimkakati, kama vile Mradi wa Bwawa la Mwl. Nyerere, ambao umeleta manufaa makubwa kwa wananchi.
Ziara hiyo iliwashirikisha viongozi mbalimbali wa chama na jumuiya zake kutoka Tanzania Bara na visiwani, na ililenga kuonyesha mafanikio ya Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan katika kuboresha miundombinu ya taifa.
Viongozi hao walisisitiza umuhimu wa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
28-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
28-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
28-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
28-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
28-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
28-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
28-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
28-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
28-10-2025
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema chama hicho kitaendelea kuthamini na kuendeleza kwa vitendo mahusiano mema ya kisiasa,kijamii na kiplomasia baina yake na chama cha kikomunisti cha China (CPC).
28-10-2025