SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt Hussein Ali Mwinyi katika hafla ya uzinduzi wa Mfumo Jumuishi wa Kielektroniki (ISQMT) uliofanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Amesema kuzinduliwa kwa mfumo Jumuishi wa Kielektroniki wa Viwango wa ZBS utatanua wigo madhubuti wa kurahisisha mchakato wa kukuza ubora wa bidhaa, kuhakikisha uwazi katika udhibiti na kurahisisha huduma kwa wazalishaji, wafanyabiashara na watumiaji kwa ujumla.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Mfumo wa Viwango wa ZBS utaiwezesha Taasisi hiyo ya Viwango Zanzibar kuwa na uwezo wa kufuatilia bidhaa kwa usahihi, kuharakisha utoaji wa vyeti vya ubora na kuwawezesha wadau wote kupata taarifa kwa njia ya kidijitali jambo litakaloongeza ufanisi katika Sekta ya Viwanda na Biashara.
Aidha, Mhe. Hemed amesema Mfumo wa ISQMT umelenga kuweka Mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa zinakuwa na ubora na zinakidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa pamoja na kuondoa usumbufu ulikuwepo kwa muda mrefu hasa katika upatikanaji wa huduma kwa uwazi.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewahimiza watendaji wa ZBS kuhakikisha kuwa Mfumo wa ISQMT unatumika kwa ufanisi mkubwa pamoja na kuwataka wafanyabiashara, Wazalishaji na wadau wote wa Sekta ya Viwango kuutumia kikamilifu mfumo huo kwa lengo la kukuza ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini.
Mhe. Hemed ametoa wito kwa wadau wote wa Sekta ya Biashara na Viwanda kushirikiana na ZBS na Taasisi nyengine za udhibiti wa viwango ili kuhakikisha kuwa bidhaa zote zinakuwa na viwango bora na salama kwa matumizi ambavyo vitaiwezesha Tanzania kuwa Taifa lenye ushindani mkubwa katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Zanzibar (ZBS) Ndugu Yusuph Majid Nassor amesema madhumuni ya Kuazimishwa kwa Mfumo wa Viwango Zanzibar ni kuleta ujumuishaji wa wadau wote wanaofanya kazi na ZBS ili kufanya kazi kwa ufanisi na Tija pamoja na kupunguza changamoto mbali mbali katika utowaji na upatikanaji wa huduma.
Yusuph amesema zaidi ya shilingi za Kitanzania Bilioni 1.2 zimewekezwa katika uandaaji wa Mfumo huo kupitia wafadhili Trade Mark Afrika ambao utarahisisha upatikanaji wa huduma kwa njia ya kidijitali kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kanda Afrika Mashariki na Kati bibi Monica Hangi amesema Taasisi ya Trade Mark Afrika kwa Kushirikiana na Shirika la Viwango Zanzibar (ZBS) wameamua kuanzisha mfumo wa viwango Zanzibar kwa lengo la kuboresha mazingira ya ubora na kuweka ufanisi katika kuboresha na kuweka viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa.
Monica anesema kuzinduliwa kwa mfumo huo Zanzibar itaweza kuunganishwa na masoko ya ndani na nje ya nchi, kufanya kazi kwa uwazi, uhakika na kwa haraka jambo ambalo litachangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali.
Monica amefahamisha kuwa mfumo huo utakaokuwa na viwango ambavyo vitawasaidia wadau na wazalishaji wa bidhaa Zanzibar kuweza kutengeneza bidhaa zenye viwango vya kufikia na kukidhi matakwa ya ushindani wa Kibiashara katika Masoko ya Biashara ya ndani na nje ya nchi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
06-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
06-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
06-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
06-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
06-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
06-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
06-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
06-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
06-12-2025
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema chama hicho kitaendelea kuthamini na kuendeleza kwa vitendo mahusiano mema ya kisiasa,kijamii na kiplomasia baina yake na chama cha kikomunisti cha China (CPC).
06-12-2025