Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
Wito huo ameutoa katika Ukumbi wa Madinat - Albahr Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar wakati akifungua mkutano wa 14 wa Mapitio na Mpango wa pamoja wa Utekelezaji katika Sekta ya Afya.
Amesema kufanya kazi kwa bidii na nidhamu ni kufuata msingi wa maadili ya kazi ya utoaji wa huduma za afya kutasaidia kupunguza malalamiko yanayotolewa na baadhi ya hudumu wakati wa kuwahudumia wagonjwa.
Mhe. Hemed amewaomba Washirika wa Maendeleo kuelekeza nguvu zao katika kuisaidia Wizara ya Afya kwa kuweka miundombinu ya kidijitali ya ukusanyaji wa taarifa za afya ili juhudi zinazochukuliwa na Serikali na Wadau ziweze kutatua changammoto ikiwemo ya upatikanaji wa taarifa sahihi za takwimu za afya.
Nae Waziri wa Afya Zanzibar Mhe Nassor Ahmed Mazrui amesema kuwa bila ya kuimarisha afya ya msingi hawatafikia malengo hivyo wataendelea kuimarisha miundombinu na vifaa tiba vya kisasa ili kutoa huduma bora kwa jamii.
Waziri Mazrui ameeleza kuwa vifo vya watoto vimepungua kutoka 1940 kwa mwaka 2023 hadi kufikia 1847 kwani lengo la Serikali ni kupunguza vifo vya mama na mtoto
Aidha amewasisitiza madaktari na wataalamu wa Afya kubuni miundombinu bora itakayoweza kuwasaidia mama wajawazito ili kupunguza kifafa cha mimba sambamba na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mkurugenzi Mkuu Wizara ya Afya Dkt Amuor Suleiman amesema kuwa kwa mwaka 2022 hadi 2024 Wizara imefanikiwa kutoa huduma za afya katika vituo vya ngazi ya chini (vituo vidogo) pamoja na kuanzisha mfuko wa huduma za afya kwa ajili ya kutoa huduma bora nchini ambapo Serikali imetenga bilioni 344 kwa Sekta ya Afya ili kuimarisha afya za wananchi.
Aidha amefahamisha kuwa Wizara imefanikiwa kuzalisha hewa tiba pamoja na kununua Magari makubwa ambayo yanatoa huduma za afya, ambulance kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii, kununua vifaa vya kugundukia maradhi yanayowakabili wananchi ikiwemo kansa Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarika.
Akizungumzia maradhi yanayoongoza hadi kufikia sasa ni pamoja na maradhi ya mfumo wa hewa, maradhi ya kuharisha pamoja maradhi ya UTI, ipo haja ya kutilia mkazo kwa mwaka ujao ili kupunguza matatizo hayo.
Dk Amour ameeleza kuwa kwa upande wa watoto chini ya miaka mitano matatizo ya mfumo wa kupumua pamoja na maradhi ya ngozi ambapo maradhi yanayoongoza kusababisha vifo ni maradhi yasiyoambukiza hivyo mikakati madhubuti inahitajika ili kupunguza idadi ya vifo hivyo ikifuatiwa na vifo vya watoto wachhanga.
Mkutano huo umewashirikisha wadau mbalimbali wa Afya wakiwemo washirika wa kimataifa ambapo Kaulimbiu ya mkutano huo ni "Uwepo wa Mfumo Bora wa Huduma za Afya ya msingi uliyoungwanishwa,ubunifu unaojengwa kwa ushahidi ili kufikia Upatikanaji wa Afya Jumuishi kwa wote”.
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
19-11-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
19-11-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
19-11-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
19-11-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
19-11-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
19-11-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
19-11-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
19-11-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
19-11-2025
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema chama hicho kitaendelea kuthamini na kuendeleza kwa vitendo mahusiano mema ya kisiasa,kijamii na kiplomasia baina yake na chama cha kikomunisti cha China (CPC).
19-11-2025