Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Sudan Kusini zimesisitiza kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuhakikisha fursa muhimu za kiuchumi zinanufaisha pande zote mbili.
Msisitizo huo umetolewa wakati Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Sudan Kusini, Mhe. Ramadan Mohammed Abdallah Goc pembezoni mwa Kikao cha 46 cha Baraza la Mawaziri la Umoja wa Afrika kilichofanyika tarehe 12 na 13 Februari, 2025 Addis Ababa, Ethiopia.
Mazungumzo ya viongozi hao yaliangazia katika masuala ya kodi hususan suala la kujengeana uwezo katika masuala ya usimamizi wa kodi ambapo, Waziri Kombo alieleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Sudan Kusini katika kuhakikisha lengo hilo linakamilika kikamilifu kwa kuinua uchumi kupitia mapato ya ndani na kujenga uwezo wa kujitegemea.
Pia, walijadili juu ya kukuza ushirikiano wa kibiashara ambapo wamesisitiza umuhimu wa wafanyabiashara wadogo na wakubwa wa nchi hizo mbili kushiriki katika maonesho ya biashara kama vile ya Sabasaba, maonesho ya wajasiriamali ya Afrika Mashariki maarufu kama ‘Juakali’, na maonesho ya kilimo ya Nanenane kwakuwa yamekuwa kiungo imara kwa wafanyabiashara kutangaza, kuuza bidhaa zao pamoja na kutengeneza mtandao na wafanyabiashara wenzao katika kukuza soko la bidhaa na huduma katika kanda na kimataifa.
Kadhalika, wamejadili ushirikiano katika masuala ya elimu ambapo Mhe, Goc ameeleza kuwa Sudan Kusini inaleta wanafunzi wa vyuo vikuu kusoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo hatua hiyo inawezesha nchi hizo mbili kukuza mawasiliano kati ya vijana wa kitanzania na wa Sudan kusini na hivyo kupelekea kukua kwa shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
26-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
26-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
26-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
26-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
26-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
26-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
26-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
26-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
26-10-2025
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dkt.Mohamed Said Dimwa,amesema chama hicho kitaendelea kuthamini na kuendeleza kwa vitendo mahusiano mema ya kisiasa,kijamii na kiplomasia baina yake na chama cha kikomunisti cha China (CPC).
26-10-2025