Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China katika mambo mbali ya Kimaendeleo ikiwemo Sekta ya Uchumi wa Buluu, Miundombinu, Mafuta na gesi.
Ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Gavana wa jimbo la JIANGSU nchini China Bwana XU KUNLIN na ujumbe wake waliofika ofisini kwake Vuga kwa ajili ya kufanya mazungumzo kufuatia kutimia kwa miaka 60 ya ushirikiano wa China na Zanzibar katika sekta ya Afya.
Amesema, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeipa kipaumbele Sekta ya uchumi wa Buluu ambayo imekuwa ikitoa fursa mbali mbali za ajira kwa wananchi hivyo amemtaka Gavana huyo kuendeleza mashirikiano katika sekta hio pamoja na Sekta nyengine ikiwemo Afya, Miundombinu, Utalii, Mafuta na Gesi.
Mhe. Hemed amesema wakati China na Zanzibar inatimiza miaka 60 ya ushirikiano katika Sekta mbali mbali ikiwemo sekta ya Afya, Zanzibar inajivunia kuendelea kupokea madaktari wa kada mbali mbali kutoka China ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii na kutoa msaada mkubwa katika masuala ya Kitabibu.
Sambamba na hayo, Makamu wa Pili wa Zanzibar amemuhakikishia Gavana XU KUNLIN kuwa Zanzibar itaendeleza ushirikiano uliopo na Serikali ya watu wa China na kuwataka kuendelea kuwekeza Zanzibar katika maeneo mbali mbali ya kiuchumi na kimaendeleo.
Kwa upande wake Gavana wa Jimbo la JIANGSU nchini china Bwana XU KUNLIN ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano wa muda mrefu kupitia Nyanja mbali mbali ikiwemo za elimu na afya .
Amesema Jimbo la JIANGSU limekuwa likipiga hatua katika mambo mbali mbali yakiwemo masuala ya Uchumi hivyo wako tayari kushirikiana na Zanzibar katika eneo hilo ili kuhakikisha inazidi kupiga hatua kwa maslahi mapana ya wananchi wa pande zote mbili.
Bwana XU KUNLIN amesema katika sekta ya Afya China itahakikisha inaendeleza ushirikiano na Zanzibar katika suala la Teknolojia katika kukinga na kutibu maradhi mbali mbali sambamba na kuwapatia Taaluma na kuwajengea uzoefu watendaji wa Wizara ya Afya .
Nae Waziri wa Afya Mhe. Nassor Ahmed Mazurui ameishukuru Serikali ya watu wa China kwa kuendelea kuisaidia Zanzibar hasa katika sekta ya Afya kwa kuleta madaktari bingwa kuja Zanzibar kwa kutoa msaada wa kitabibu kila mwaka na kuwajengea uwezo madaktari wazawa .
Mhe. Mazurui amesema Miaka 60 ya ushirikiano katika sekta ya Afya kwa Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China umeleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo katika sekta ya hio ikiwemo kuboreshwa kwa upatikanaji wa huduma kuanzia Vituo vya Afya hadi Hospitali ya Rufaa zilizopo nchini.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
28-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
28-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
28-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
28-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
28-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
28-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
28-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
28-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
28-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
28-10-2025