DK. MWINYI AMEFUNGUA SKULI YA KIDONGOCHEKUNDU MSINGI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema miaka 59 ya Muungano wa Tanzania imeleta Mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Elimu kwa pande zote ikiwemo kuboresha miundombinu ya majengo ya kisasa na huduma zenye ubora katika kutoa ufaulu mzuri kwa wanafunzi.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo kwenye sherehe za ufunguzi wa Skuli ya msingi ya kisasa Kidongochekundu iliopo kwenye jimbo la Jang’ombe, Wilaya ya Mjini ikiwa ni shamrashamra za miaka 59 ya Muungano wa Tanzania.
Alisema, Zanzibar kwasasa inastahiki kuwa na skuli za msingi za ghorofa zenye ubora wa hali ya juu ili kuendana na hadhi ya miaka 59 ya Muungano wa Tanzania ambapo Serikali zote mbili ya Muungano wa Tanzania na ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeshuhudia ongozeko kubwa la taasisi nyingi za elimu na wanafunzi wengi.
Alisema, kabla ya Muungano wa Tanzania, sekta ya elimu ilikua na wanafunzi 25, 000 na sasa idadi imeongezeka kufikia 570,000.
Akizungumzia miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi alisema Serikali ina mpango wa kuongeza madarasa 1000 yenye miundombinu na vifaa vya kisasa zikiwemo maabara, vyumba vya kompyuta, maktaba, vyoo vya kisasa na ofisi za walimu pamoja na kufungua miradi mikubwa zaidi ya maendeleo.
Alisema mabadiliko ya elimu Zanzibar yatafikiwa kwa kuwa na ujenzi imara wa miundominu ya majengo ya kisasa yatakayochukua wanafunzi wachache kwenye madarasa, vifaa vya kisasa na mazingira mazuri ya kufundisha na kujinza.
Rais Dk. Mwinyi aliongeza skuli ya Kidongochekundu Msingi ni miongoni mwa mfano hai wa skuli zote za msingi anazotaka kuzijenga Zanzibar hadi kufikia Januari, 2025 pamoja na kukamilisha miradi mengine mikubwa ya maendeleo ili kuendana na hadhi ya miaka ya Mapinduzi ya Zanzibar na miaka 59 ya Muungano wa Tanzania.
“Skuli hii ni mfano wa skuli zetu za msingi nnazotaka ziwe nchini, skuli za ghorofa ambazo ndani yake mna maabara za sayansi, maktaba, vyumba vya kompyuta na madarasa wanafunzi wetu wasiozidi 45” alielekeza Dk. Mwinyi
Alisema serikali itafanya kila jitihada kuhakikisha Zanzibar inapata madarasa ya kutosha, nyenzo bora za kusomea ikiwemo kufanikisha skuli kuwa na mkondo mmoja badala ya miwili kama awali. Aidha, aliwataka watendaji wa wizara ya elimu kuhakikisha skuli inatoa huduma zinazoendana na hadhi yake kwa kutoa ufaulu mzuri kwa wanafunzi.
Naye, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Mohamed Mussa alisema ujenzi wa skuli hiyo ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya 2020/2025 ambapo serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliahidi kujenga miradi malimbali ya maendeleo.
Alieleza Wizara ya Elimu imepiga hatua kubwa katika kukamilisha miradi yote iliyopanga na kwamba imeakisi dhima ya miaka 59 ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Katibu Mkuu wizara ya Elimu, Khamis Said alisema ujenzi wa skuli hiyo umegharimu shilingi bilioni 4.466 ambao umejumuisha Maktaba, Maabara, chumba cha kompyuta, ofisi ya mwalimu kuu, ofisi ya msaidizi mwalimu mkuu, ofisi tatu za walimu, chumba cha kusalia, vyoo 25 , viti na meza 1305 kwaajili ya wanafunzi wote.
Skuli ya Msingi Kidongochekundu ni miongoni mwa skuli mpya zilizojengwa na Serikali ya awamu ya nane kwa fedha za ahuweni ya uviko 19 Zanzibar, kwa Unguja na Pemba.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
31-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
31-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
31-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
31-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
31-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
31-12-2025