MWINYI KUJENGA KIWANJA CHA KISASA TUMBATU
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amekubali ombi lilotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi Hamza Hassan Juma kupitia TASAF juu ya mpango wa kujenga kiwanja cha kisasa cha michezo katika kisiwa cha Tumbatu.
Rais Dk. Mwinyi aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Tumbatu Jongowe ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Rais Mwinyi aliwapongeza kwa kuja na wazo hilo na kuahidi kwamba wakishafika hatua nzuri basi ataweka nyasi bandia ili kuona vijana wanacheza katika mazingira mazuri.
Mapema, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Shughuli za Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma, alisema kuwa kwa kushirikiana na TASAF wana mpango wa kujenga kiwanja Maalum cha mpira katika Kisiwa cha Tumbatu kama ni sadaka yao katika kisiwa hicho ili kuwawekea mazingira mazuri ya michezo vijana wa kisiwa hicho.
Alisema kuwa atakaa na viongozi wa Jimbo hilo kwa kushirikiana nao katika kuona vijana wa kisiwa hicho wanapata kiwanja kwa ajili ya michezo ikiwemo mchezo wa mpira wa miguu.
Hivyo, alimuomba Rais Mwinyi kushirikiana katika ujenzi huo kwa kuwatilia nyasi bandia kama alivyoahidi katika maeneo mengine ikiwemo viwanja vya Mjini.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
30-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
30-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
30-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
30-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
30-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
30-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
30-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
30-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
30-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
30-12-2025