CDE. MBETO NA CDE. KILUPI WAWAPIGA MSASA MATIBU WA SIASA NA UENEZI ZANZIBAR
MAKATIBU wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar wametakiwa kuwa wabunifu na wachapakazi katika kueneza na kutangaza utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Rai hiyo imetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar Ndg.Khamis Mbeto Khamis wakati akizungumza na makatibu hao wa ngazi za majimbo hadi mikoa huko Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar.
Amewakumbusha makatibu hao kuwa wanatakiwa kutangaza utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 inayotekelezwa katika maeneo yao.
Alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya awamu ya nane chini ya uongozi wa Rais Dk.Mwinyi inatekeleza kwa ufanisi mkubwa Ilani ya CCM.
Katika maelezo yake Mbeto,aliwambia watendaji hao kuwa wanatakiwa kubadilika kiutendaji na kufanya kazi kwa bidii ili waende sambamba na kasi ya CCM kiutendaji.
“Makatibu nyinyi ndio mdomo wa Chama chetu mliopewa dhamana ya kusema na kufafanua mambo yote mazuri yanayofanywa na Chama pamoja na Serikali zetu kwa ujumla.
Tuna kazi kubwa ya kueneza na kuwambia wananchi mafanikio yanayopatikana katika maeneo yenu kunajengwa barabara za lami,maji safi na salama,hospitali zenye hadhi ya kimataifa,shule za kisasa na mengine mengi yanayotakiwa kujulikana kwa umma.” alieleza Mbeto,
Alisema wananchi wanatakiwa kujua kwa kina utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na CCM katika kampeni za uchaguzi mkuu uliopita ili wajiridhishe.
Alisema Zanzibar inaendelea kupiga hatua kubwa katika sekta za utalii,afya,kilimo,uvuvi,maji safi na salama,miundombinu ya umeme,usafiri wan chi kavu na baharini,usafiri wa anga,uwezeshaji wananchi kiuchumi pamoja na ustawi wa jamii.
Pamoja na hayo alieleza kuwa CCM itaendelea kufanya siasa za kisayansi zinazobeba dhana ya kumiza ahadi kwa vitendo badala ya maneno.
Naye Katibu wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Organaizeshe CCM Zanzibar Ndg.Omar Ibrahim Kilupi, alisema kipaumbele chake ni kutekeleza ibara ya tano ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2022,kuhakikisha Chama kinashinda kwa kishindo kwa kila uchaguzi.
Alisema ushindi wa CCM utapatika kutokana na juhudi kubwa za kutangaza fursa na maendeleo yanayofanywa na serikali ili wananchi wajue na kuendelea kujenga imani kwa Chama walichokipa ridhaa ya kuongoza dola.
Kupitia kikao hicho Ndg.Kilupi, aliwataka wabunge,wawakilishi na madiwani kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi majimboni.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
30-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
30-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
30-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
30-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
30-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
30-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
30-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
30-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
30-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
30-12-2025