RAIS DK.MWINYI ASAINI SHERIA MPYA ZINAZOGUSA WANANCHI NA HAKI ZAO
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema kusainiwa kwa sheria mpya itaondoa changamoto ambazo zilikuwa vikwazo katika kufikia malengo ya kimaendeleo.
Amesema sheria hizo mpya ni Sheria mpya ya Mahkama ya Kadhi Zanzibar, Sheria mpya ya Ukaguzi wa Umma, Sheria mpya ya Uwekezaji Zanzibar, ambayo ni sheria bora kwa mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji nchini, Sheria ya kuweka masharti ya utoaji leseni udhibiti na usimamizi wa huduma ndogo za fedha kwa ajili ya kudumisha utulivu, usalama na ubora wa huduma hizo.
Rais Dk.Mwinyi amesema hayo wakati wa hafla ya utiaji saini wa sheria mpya nne viwanja vya Ikulu Zanzibar tarehe: 01 Februari 2024.
Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Sheria zilizosainiwa zimepita katika hatua mbalimbali ikiwemo kufanyika kwa utafiti wa kina na ukusanyaji wa maoni ya wadau Unguja na Pemba kabla ya kuwasiilishwa Baraza la Wawakilishi na kujadiliwa kwa mfumo wa demokrasia shirikishi.
Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa ni jambo la kihistoria kusainiwa kwa sheria mpya nne hadharani kwa wakati mmoja.
Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amesema Sheria zote nne zilizosainiwa zinagusa moja kwa moja maslahi ya wananchi na haki zao ikiwemo kuimarisha miongozo ya mifumo jumuishi ya kusimamia shughuli zote za uwekezaji, kupanua wigo wa kazi za ukaguzi ili kufikia ngazi za kitaifa na kimataifa, kubaini na kuzuia matumizi mabaya ya fedha za umma, kukabiliana na vitendo vya rushwa, kuzuia matumizi mabaya ya mifumo inayoathiri utekelezaji wa kazi za ukaguzi.
Rais Dk.Mwinyi amezitaka taasisi za sheria kufanya mapitio sheria zinazokwaza kasi ya maendeleo katika maeneo ya mafuta na gesi asilia.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
20-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
20-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
20-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
20-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
20-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
20-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
20-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
20-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
20-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
20-10-2025