DK. MWINYI - SASA NI WAKATI WA KUJENGA CHAMA CHETU
Makamo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar, ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema wakati umefika CCM kutumia rasilimali za Chama zilizopo ili kuendelea kujiwezesha kiuchumi ikiwemo kutatua changamoto za uchakavu wa majengo na posho kwa watendaji.
Akizungumza na watendaji wa ngazi mbalimbali wakiwemo mabalozi, wajumbe wa halmashauri ya mkoa wa magharibi Kichama ikiwa ni mara ya kwanza tokea kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar hafla ambayo ilifanyika katika ukumbi wa Piccadilly Kombeni
Alisema, kumekuwa na rasilimali nyingi katika chama lakini bado hazijatumika ipasavyo hali inayochagia kuwepo kwa maslahi duni ya watendaji hivyo amewataka watendaji kulisimamia suala hilo ili kuona masuala hayo yanakaa sawa.
Aidha aliwataka viongozi wa majimbo kurudi katika majimbo yao kwani kumekuwepo baadhi ya viongozi hao, kugombana wenyewe kwa wenyewe jambo ambalo linaharibu utekelezaji wa ilani ndani ya jimbo na kupelekea kuwagawa wanachama, hivyo ameitaka sekretariet ya chama kuwaita kabla ya kusubiri siku za uchaguzi kufika
Akizungumzia makundi ndani ya Chama, Dk. Mwinyi, amewataka wanachama kuachana na makundi na waendelee kufanya kazi kwa ushirikiano kwani makundi yamekuwa yakiathiri chama.
Pamoja na hayo, aliiagiza sekretariet ya chama kuandaa mafunzo kwa viongozi wa chama waliochaguliwa kupitia ngazi zote ili kutambua wajibu wao na majukumu yao ya kiutendaji.
Aliwataka viongozi hao, kuengeza wanachama wapya pamoja na kuhamasisha na ulipaji wa ada ili kuimarisha uhai wa chama kwani uhai wa chama ni kuengeza idadi ya wanachama wapya.
Akizungumzia utekelezaji wa ilani, Rais.Dk. Mwinyi, alisema ilani ya mwaka 2020-2025 kwa sasa imefikia nusu kwani katika kipindi cha miaka miwili miradi mbalimbali wameitekeleza ikiwemo huduma za kijamii, ikiwemo Afya, Elimu, barabara na huduma za maji safi na salama ambapo baadhi ya sekta zimeshavuka lengo lililoelekeza katika ilani ya uchaguzi.
Akimkaribisha Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Naibu, Katibu wa Chama cha CCM Zanzibar, Dk. Mohamed Said Mohamed ( Dimwa), alisema, CCM hakitajibu maneno ya wanaotaka kuchafua amani ya nchi hivyo CCM itaendelea kujibu kwa hoja vitendo ikiwemo kuwapatia wananchi maendeleo yaliyofikiwa nchini chini ya uongozi wa Rais, Dk. Mwinyi.
"CCM, hatutajibu porojo zao wapinzani sisi kawaida yetu tunatekeleza ilani ya CCM na majibu yetu nyote tunajibu kupitia maendeleo yaliyofikiwa chini ya uongozi wa makamu mwenyekiti wetu" alisema.
Pamoja na hayo, aliwasihi baadhi ya viongozi kuacha kuwabeba mikoba wagombea wakati bado wa uchaguzi haujafika na kusisitiza kuachwa viongozi waliokuwepo kufanya kazi ya utekelezaji wa ilani na endapo kiongozi atakayebainika hativumiliwa katika chama.
"Wakati wa demokrasia ikifika watakuwa na haki ya kuendelea kugombea na hatozuiliwa mtu yoyote ila kwa sasa tutakula nao sahani moja"
Akitoa salam za Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkuu wa Mkoa huo, Idrissa Kitwana Mustafa, alisema Serikali ya mkoa imekuwa ikishirikiana na serikali hasa katika utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020-2025 katika upatikanaji wa maendeleo kwa wannachi wote bila ya ubaguzi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
14-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
14-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
14-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
14-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
14-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
14-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
14-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
14-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
14-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
14-12-2025