Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema kuna kila sababu ya Jimbo la Mtambwe kubaki katika Ngome ya Chama cha Mapinduzi katika ngazi zote za Uongozi ifikapo Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Akizungumza na wana CCM na wananchi wa Jimbo la Mtambwe huko katika viwanja vya kisiwani Mhe. Hemed amesema Chama kinahitaji kuimarishwa na kusimamiwa vizuri katika Jimbo hilo kwa kuongeza nguvu za kuwashawishi wananchi wa Mtambwe ili waweze kuendelea kujiunga kwa wingi na CCM.
Ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi kina dhima kwa wazanzibari kuwatumukia kupitia ahadi walizoweka kama maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi inavyoeleza ambapo SMZ chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi itatatua changamoto zote zinazowakabili wazanzibari.
Amewataka Viongozi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba kuendelea kutangaza mazuri yanayofanywa na Chama cha Mapinduzi na kuachana na siasa za chuki na uhasama badala yake washirikiane katika kuinadi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kuitekeleza kwa vitendo jambo ambalo litatoa wigo mkubwa kwa wananchi wa mtambwe hususan wapinzani wavutiwe na hatimae kujiunga na CCM.
Amewataka Viongozi kuwa na uzalendo wa Nchi yao kwa kuipigania na kuitetea Nchi yao sambamba na kujipanga katika kushinda kwa kishindo katika Jimbo laTambwe na Majimbo yotess ya Zanzibar.
Amesema ili kuleta mabadiliko majimboni ni lazima Viongozi kuwa wabunifu katika kuunda miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itawapatia vijana kujiajiri na kuwaweka pamoja katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Mberwa Hamad Mberwa ameeleza Mjumbe huyo wa Kamati Kuu kuwa Kamati ya Siasa Mkoa na Wilaya zitahakikisha zinasimamia maelekezo aliyoyatoa na kuyafanyia kazi kwa ngazi zote kuanzia Mkoa hadi Shina
Amemuhakikishia kuwa Mkoa wa Kaskazini Pemba utakuwa ni wa mfano kwa kura nyingi za CCM ukifika Uchaguzi wa Dola wa mwaka 2025 kutokana na utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika Majimbo yote ya Mkoa huo.
Muwakilishi wa Jimbo la Micheweni na Waziri wa Kilimo Maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Shaame Khamis ameeleza kuwa Serikali imejenga masoko kila Mkoa ili kurahisisha uuzaji wa biashara zinazotoka mashambani kwa ubora na kwa bei za uhalisia. ss
Nae Mkuu wa Mkoa wa Kaskazi Pemba Salama Mbarouk Khatib amempongeza Mhe.Hemed kwa uamuzi wake wa kufanya ziara ya kukiimarisha chama ambapo wanaamini matunda ya ziara hiyo yataonekana kwani mabadiliko makubwa yenye tija yatatapatikana ndani ya chama cha Mapinduzi na Serikali kwa ujumla.
Ameeleza kuwa wataendelea kufanya ziara mara kwa mara ili kuhakikisha CCM inajengeka na kuendelea kuwa imara na kuingiza wanachama wengi watakaokuja kukipatia Chama hicho ushindi ifikapo mwaka 2025
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
13-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
13-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
13-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
13-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
13-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
13-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
13-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
13-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
13-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
13-12-2025