DK. MWINYI AISHUKURU MAREKANI KUSAIDIA SEKTA YA AFYA NCHINI
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi ametoa wito kwa wadau mbalimbali kutambua umuhimu wa ushirikiano ili kufikia malengo kwa kuwekeza rasilimali fedha katika kuimarisha utafiti, kuboresha miundombinu ya afya, na kuhakikisha upatikanaji matibabu sawa kwa wagonjwa wa saratani nchini.
Rais Dk.Mwinyi amesema hayo katika jukwaa la uwekezaji linalolenga kuimarisha huduma za saratani nchini, ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam tarehe:06 Februari 2024.
Vilevile Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa kupitia ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, watafiti na wataalamu wa tiba kunaweza kubadilisha taswira za huduma za matibabu ya saratani nchini.
Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali imeanza kuchukua hatua kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo saratani kwa kujenga miundombinu ya huduma za afya, mikakati ya upatikanaji wa huduma bora za matibabu bora kwa wote.
Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameishukuru Serikali ya Marekani kwa ushirikiano wao kufanikisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo ikiwemo sekta ya afya nchini.
Pia amewashukuru wadau wa Global Health Catalyst ambao wamejitolea kushirikiana na Serikali katika mapambano ya maradhi ya saratani, wawekezaji wa ndani wakiongozwa na Taasisi ya sekta binafsi Tanzania (TPSF) pamoja na CEO Roundtable kwa utayari walionyesha kushirikiana na Serikali.
Rais Dk.Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwa uongozi na jitihada zake za kuimarisha ustawi wa maendeleo nchini
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
23-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
23-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
23-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
23-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
23-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
23-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
23-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
23-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
23-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
23-12-2025