SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR IMEAHIDI KUSAIDIA VIKUNDI VYA KINA MAMA ILI VIWEZE KUPATA MIKOPO NA KUJIKWAMUA KIMAISHA
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ametoa kauli hiyo alipofanya mazungumzo na Uongozi wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) waliofika kujitambulisha Ofisini kwake Vuga Jijini Zanzibar.
Mhe. Hemed ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amesema Serikali inatoa Mikopo ya gharama nafuu kwa vikundi vya wajasiriamali kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kuwaahidi kina mama kuwa Serikali inatoa kipaumbele kwa wanawake ili waondokane na utegemezi.
Mhe. Hemed ameeleza kuwa dhamira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kutenga fedha kwa ajili ya mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali ni kuweza kuwasaidia wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa urahisi na kuweza kujikimu kimaisha.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed ameupongeza Uongozi wa UWT kwa kuandaa mpango kazi ambao umelenga kuiletea mabadiliko Jumuiya hiyo hasa mpango wa kuanzisha vitega uchumi kwa kila Mkoa hatua ambayo itasaidia Jumuiya hiyo kuacha utegemezi katika kuendesha shughuli za kila siku.
Amesema, Chama Cha Mapinduzi kimeelekeza kuboresha vitega uchumi na kubuni vyanzo vipya vya mapato kwa Jumuiya zake ili kurahisisha uendeshaji wa shughuli za Chama za kila siku.
Pamoja na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewapongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea maendeleo watanzania ndani ya kipindi cha muda mfupi.
Aidha Mhe. Hemed amewasihi viongozi hao kuwa wavumilivu na kutovunjika moyo kwa changamoto mbali mbali wanazokumbana nazo katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania Bi. Zainab Shomari amemueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kuwa UWT imejipanga kufanya mabadiliko kwa kujiimarisha kimaendeleo kiutendaji, kisiasa na kiuchumi.
Aidha ameeleza kuwa Umoja wa Wanawake Tanzania umefurahishwa kwa juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kujenga Hospital zenye huduma za Mama na Mtoto hatua ambayo itasaidia kumaliza changamoto ya usumbufu wa kina mama wanapofata huduma hizo na kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
21-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
21-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
21-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
21-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
21-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
21-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
21-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
21-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
21-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
21-12-2025