WAZEE WA CCM WATOA NENO KWA DK. MWINYI
BARAZA la wazee la Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar limempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kupandisha pensheni kwa wastaafu kwa asilimia 100 ambapo utaratibu huo mpya unatarajia kuanza ifikapo Julai mwaka mpya wa bajeti utakapoanza.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisini kwao Ofisi Kuu za CCM Kisiwandui mjini Unguja Mwenyekiti wa Baraza hilo Khadija Jabir Mohamed alisema Baraza la wazee limepokea taarifa hiyo kwa furaha kubwa kwa kuona kuwa bado Rais Dk.Mwinyi anaendeleza azma na malengo ya mapinduziya kuhakikisha wazee wanatunzwa.
"Kama mnavyokumbuka katika kilele cha sherehe za maadhimisho ya siku za wafanyakazi zilizofanyika viwanja vya skuli ya Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo Rais Dk.Mwinyi alikuwa mgeni rasmi na aliahaidi kupandisha pensheni kwa wastaafu kwa wastaafu wa kima cha chini kufikia sh.180,000 kutoka sh.90,000 hii kwetu ni tunajivunia sana,"alisema
Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo alisema mbali na hilo pia Baraza la wazee linampongeza Rais Dk.Mwinyi kwa kupandisha pensheni jamii kwa asilimia 150 kwa wazee kuanzia miaka 70 ambapo wanatarajia kupokea sh.50000 kutoka sh.20000 ambayo wanayopokea hivi sasa.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CCM Zanzibar Haji Machano Haji alisema hatua hiyo iliyofanywa na Rais Dk.Mwinyi ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ambapo katika ibara ya 214 inaeleza kuwa CCM inatambua umuhimu wa wazee katika Taifa letu na itaendeleakuwapatia huduma za kijamii na kisheria.
"Kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ibara 214 CCM inaielekeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kipindi cha miaka mitano ijayo Kutekeleza mpango wa pensheni jamii kwa wazee wenye umri wamiaka 70 na kuendelea kwa kuongeza bajeti ya mpango kutokash.bilioni 6.5 hadi sh.bilioni 7 kwa ajili ya malipo ya wazeewalioongezeka Unguja na Pemba,"alisema
Katibu huyo alisema ikiwa Baraza hilo la wazee ni miongoni mwa wazee ambao wananufaika na pensheni hiyo wazee hao wanampongeza Rais Dk.Mwinyi kwa uamuzi huu wa kuongeza kiasi hicho cha pesa kwa wazee na kwamba bado baraza hilo lina imani naye kubwa kwa kuwatunza wazee wa Zanzibar.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
22-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
22-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
22-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
22-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
22-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
22-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
22-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
22-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
22-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
22-12-2025