SOKO LA UHAKIKA ZAO LA MWANI ZANZIBAR
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amemhakikishia Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. David Conar na ujumbe wake kuwa Serikali ya Zanzibar iko tayari kushirikiana na Nutri-Sun Limited kutoka Uingereza katika kukamilisha mradi wa kiwanda cha kuchakata mwani kilichopo Chamanangwe, Pemba ambacho kukamilika kwake kutawanufaisha kwa kurahisisha kupata soko la uhakika.
Katika salamu zake naye Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Conar amemweleza Rais Dk. Mwinyi kwamba mipango ya kupata mashine na teknolojia ya kuchakata mwani imekamilika hivyo ifikapo mwishoni mwa mwaka 2024 kiwanda hicho kitaanza kuzalisha “Carrageenan” ambayo itatatumika kwa matumizi ya viwanda vya chakula na matibabu.
Aidha, Bi. Marisa Drew kutoka benki ya Standard Chartered alimhakikishia Rais Dk. Mwinyi upatikanaji endelevu wa fedha ambazo zitatumika kununulia mashine na zao la mwani, kiwanda hicho kitawawezesha wakulima wa mwani hasa wanawake na vijana kujikwamua kiuchumi.
Rais Dk.Mwinyi amekutana na ujumbe huo leo tarehe: 19 Februari 2024 Ikulu Zanzibar
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
31-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
31-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
31-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
31-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
31-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
31-12-2025