Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano uliopo baina ya Zanzibar na Jamhuri ya watu wa China kwa maslahi mapana ya wananchi wa pande zote mbili .
Ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na Naibu Gavana wa Jimbo la ZHEJIANG Bwana. YANG QINGJIU na ujumbe wake waliofika ofisini kwake Vuga kumtembelea.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China katika kuisaidia Zanzibar kupitia nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya Afya, Kilimo, Elimu na Habari pamoja na miradi mbali mbali ya kimkakati jambo lililopelekea kuimarika kwa huduma katika sekta hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameishukuru Serikali ya Jamuhuri ya watu wa china kwa kuendelea kuisaidia Zanzibar kupitia Nyanja mbali mbali ikiwemo kupokea madaktari Bingwa kutoka nchini China ambao husaidia kutoa huduma za tiba na ushauri kwa wagonjwa wanaofika katika hospitali mbali mbali ndani ya Visiwa vya Unguja na Pemba.
Aidha, Mhe. Hemed amemueleza kuwa kipaombele cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni Uchumi wa Buluu ambao unajumuisha mambo mbali mbali ikiwemo Sekta ya Utalii ambayo imekuwa ikiichangia pato kubwa la Serikali kutokana na ongezeko la wageni wengi wanaoitembelea Zanzibar.
Sambamba na hayo, Mhe.Hemed ameikaribisha Serikali ya Jamuhuri ya watu wa China kupitia uongozi huo wa Jimbo la ZHEJIANG kuja kuekeza Zanzibar na kuzitumia fursa mbali mbali zilizopo nchini ikiwemo uchumi wa buluu.
Nae Naibu Gavana kutoka Jimbo la ZHEJIANG nchini China Bwana. YANG QINGJIU amesema wameamua kuja Zanzibar kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili hasa katika masuala ya maendeleo.
Bwana. YANG QINGJIU amesema China imekuwa ikishirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya uchumi, Utamaduni na elimu kwa kuwapatia wazanzibari ufadhili wa masomo ya muda mrefu na mafunzo ya muda mfupi hasa katika kada mbali mbali kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwaongezea maarifa watumishi wa umma.
Amesema Jimbo la ZHEJIANG limepiga hatua kubwa sana katika masuala ya biashara hivyo kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanawawekea mazingira mazuri kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
26-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
26-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
26-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
26-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
26-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
26-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
26-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
26-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
26-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
26-10-2025