CCM TUMEIMARIKA ZAIDI - DK. DIMWA
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM)Zanzibar kimewataka watendaji wake kujiimarisha na mabadiliko ya mienendo ya hali ya siasa inavyokwenda.
Akizungumza katika ziara ya sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM,Zanzibar mkoa wa Kaskazini Unguja,Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Zanzibar Dk. Mohammed Said Mohammed 'Dimwa'.
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema CCM pamoja na jumuiya zake zinapaswa kujithatiti,kujijenga na kujijenga kuwa na uwezo mpya wa kulingana na uzito wa mapambano ya kisiasa yaliyopo.
"Siasa zetu zimeanza kubadilika sana na wala si siasa za kwenye majukwaa hivi karibuni juzi ACT-Wazalendo walisema tunamsubiri Dk.Dimwa ajibu hoja nasema tutajibu hoja kwa hoja tena tuna joja nyingi za kujibu," alisema
Alisema katika hilo hoja hizo haitaitoa kwenye reli CCM katika kutekeleza ilani ya uchaguzi.
"Wanazungumza suala la ujenzi wa uwanja wa Amani kuwa fedha zinazotoka wapi bila ya kupitishwa na Baraza la Wawakilishi lakini wawakilishi watakuwa wanajua kuwa kuna mfuko wa serikali ambao unaitwa mfuko wa hazina ndio kazi yake hii,"alisema
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema yeye ana uzoefu wa suala hilo kutokana na kuwa ameshawahi kuwa Mwakilishi kwa hivyo anatambua jambo hilo na kwamba atawajibu hoja kwa hoja na si kujibu mambo mengine.
Alisema CCM itaendelea kuhubiri amani ili Zanzibar iendelee kubaki na amani na kuachana na maneno ya wapinzani yanayoashiria uvunjifu wa amani.
Pia,alisema, vyama vya siasa muda wote vinatakiwa kuhubiri amani kutokana na kuwa ikitoweka haiwezi kurudi tena, na kwamba CCM itaendelea kuhubiri amani.
"Licha ya kuwa vyama vyengine vya siasa vimekuwa vikihubiri uvunjifu wa amani lakini sisi hatutahubiri masuala hayo na tutaendeleza amani ya nchi iliyopo ili tuweze kupeleka maendeleo kwa wananchi wote bila ya kubagua," alisema.
Alisema CCM itaendelea kujibu hoja kwa hoja ambazo serikali inayoongozwa na CCM imefanya maendeleo ikiwemo, kujenga shule za kisasa za ghorofa.
Mbali na hilo,Naibu Katibu Mkuu huyo aliwataka viongozi wa CCM kuendelea kutangaza maendeleo yanayofanyika kupitia ilani ya uchaguzi ya CCM inavyotekelezeka kwa wananchi.
"Tuna kila sababu ya kutembea kifua mbele, awahamasishe wanaCCM kuyatangaza mafanikio yanayotekelezwa chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi,"alisema
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
19-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
19-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
19-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
19-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
19-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
19-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
19-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
19-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
19-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
19-12-2025