AnuaniKisiwandui, Zanzibar
Simu(+255) 26 23 22965

Habari na Matukio Mbalimbali


RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA MWENYEKITI WA MAMLAKA YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU ZA TAIFA YA OMAN DR.HAMED MODH AL DHAWIANI IKULU ZANZIBAR LEO

alternative

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk. Hussein Ali Mwinyi ameiomba Serikali ya Oman kusaidia upatikanaji wa mafunzo kwa watendaji wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi.
 
Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Nyaraka na Kumbukumbu za Kitaifa ya Oman, Dk. Hamad Mohammed Al-Dhawyani aliyefika Ikulu Zanzibar kwa lengo la kuendeleza ushirikiano kati ya nchi mbili hizo, hususan suala la uhifadhi wa nyaraka na kumbukumbu za Taifa.

Habari Nyingine
Albamu