DK. MWINYI AMFUKUZA MKANDARASI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amemsimamisha kazi Mkandarasi wa Kampuni ya Associated Investment Company Ltd ya Tanzania inayojenga skuli ya Sekondari ya Mtopepo Zanzibar.
Rais Dk. Mwinyi amechukua hatua hiyo baada ya kuona uwezo mdogo wa ujenzi unaoendeshwa na Kampuni hiyo ya Associated Investment Company Ltd ya Dar es Salaam kwa kukengeuka mashari ya ujenzi na hivyo, kuona haja ya kuvunja mkataba wa ujenzi na Kampuni hiyo.
Katika maelezo yake, Rais Dk. Mwinyi alieleza kwamba Kampuni hiyo tayari imeshachukua muda wa miezi sita lakini bado haijafikia hatua za ujenzi kama ilivyokubaliana na Serikali na kushangazwa kuomba miezi mengine sita.
Alisema kuwa Kampuni hiyo haifai kufanya kazi kwani haina sifa huku akishangwazwa na Mshauri Elekezi, Kampuni ya “Edge Consultacy Company” kushindwa kuishauri Serikali jinsi ya utendaji kazi mbovu wa Kampuni hiyo na kueleza kwamba Kampuni zote hizo hazina sifa wala uwezo.
Rais Dk. Mwinyi alisema kwamba ujenzi wa mradi huo umefikia hatua hiyo kutokana na Wizara husika ya Elimu na Mafunzo ya Amali kutokuwa na muhali katika kusimamia miradi ya Serikali.
Hata hivyi, Rais Dk. Mwinyi alitioa maelekezo kwamba Mkandarasi huyo asipewe mradi mwengine wa aina yoyote kwani hana sifa wala vigezo.
“Kampuni haina uwezo, Kampuni haina bondi na Wizara ya Elimu ndio mmetufikisha hapa na hii ndio inatokana na yale maneno yanayosemwa kwamba Rais kasema apewe kazi.....huyu hafai”, alisema Dk. Mwinyi.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alisisitiza haja ya kuchukua hatua kwa kampuni iliyopewa kazi pale inapoonekana utekelezaji wa miradi ya maendeleo haiendi kama ilivyokusudiwa.
Hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliwahakikishia wananchi, walimu pamoja na wanafunzi wa skuli hiyo mpya ya Sekondari ya Mtopepo kwamba Serikali itahakikisha inafanya juhudi za makusudi ili wakati wa sherehe za Mapinduzi za Januari 12, mwakani skuli hiyo inafunguliwa.
Rais Dk. Mwinyi alieleza kwamba lengo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanziar ni kupunguza idadi ya wanafunzi wengi madarasani na ndio maana hatua za makusudi zinachukuliwa katika kuhakikisha hilo linafanikiwa na kuwataka walimu na wanafunzi kuwa na subira.
Mara baada ya kuweka jiwe la msingi la Soko la Wajasiriamali linalojengwa kwa fedha za UVIKO-19 huko Shehia ya Munduli, Rais Dk. Mwinyi aliiitaka Idara ya Manispaa Magharibi ‘A’ kubadilika na kujikita katika suala la kibiashara kwa kutafuta fedha na kuongeza Vizimba katika soko hilo ili kuleta ustawi wa biashara.
Aliiomba Benki ya CRDB kuendelea kushirikiana na Serikali na kuwakopesha fedha wajasiriamali ili waweze kuendeleza biashara zao, huku akiahidi kuongezewa kiwango zaidi cha mitaji vikundi vitakavyofanikiwa kurejesha mikopo ya awali.
Aidha, Dk. Mwinyi alipata fursa ya kutembelea na kuona maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Maji katika eneo la Masingini (Masingini Scheme) unaojengwa na Mkandarasi kutoka Kampuni ya L&T Construction kwa gharama ya Dola Milioni 35.8, mradi unaohusisha ujenzi wa matangi mawili ya maji yenye uweezo wa ujazo wa Lita Milioni 18.
Akizungumza na wananchi wa maeneo ya mradi, Dk. Mwinyi alimpongeza Mkandarasi huyo kwa kuendelea na mradi huo vizuri na kuwataka watendaji wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuhakikisha miundombinu hiyo inaleta matumaini mema kwa wananchi juu ya upatikanaji wa huduma hiyo.
Katika hatua nyengine, Rais Dk. Mwinyi alipongeza mafanikio yaliofikiwa katika utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo ya Magharibi ‘A’ , kupitia sekta za Maji, Afya, Elimu, Barabara pamoja na soko la Wajasiriamali na kusema anaridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo, mbali na kasoro iliojitokeza kwa Mkandarasi anaejenga mradi wa Skuli ya Sekondari Mtopepo.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
20-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
20-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
20-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
20-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
20-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
20-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
20-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
20-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
20-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
20-12-2025