Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imo mbioni kukimaliza Kiwanda cha kuchakatia mwani kilichopo Chamanangwe Mkoa wa Kaskazini Pemba ambacho kitakuwa ni sulihisho la kilio cha Wakulima wa Mwani Kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imo mbioni kukimaliza Kiwanda cha kuchakatia mwani kilichopo Chamanangwe Mkoa wa Kaskazini Pemba ambacho kitakuwa ni sulihisho la kilio cha Wakulima wa Mwani Kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Ndugu Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo akizungumza wanachama wa CCM na Wananchi wa Jimbo la Pandani na Jimbo la Kojani akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha Chama Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Amesema katika kutekeleza Ilani ya CCM Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa Kiwanda cha kusarifia Mwani kilichopo Chamanangwe Mkoa wa Kaskazini Pemba ambacho kitawanufaisha Wakulima wa Mwani na kitatoa fursa nyingi za ajira kwa wananchi.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itahakikisha zao la mwani linauzwa kwa bei ya juu hapa hapa Nchini hivyo amewataka Wananchi wa kisiwani Pemba waitumie vyema fursa hiyo ili kujikwamua na ukali wa maisha.
Aidha ameeleza kuwa wakulima wa zao la mwani Serikali kupitia mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi itawawezeshwa vifaa vyote vya kulimia mwani ikiwemo Kamba na Taitai ili waweze kulima bila ya kikwazo chochote.
Amesema anatambua kuwa Mkoa wa kaskazini Pemba ni maarufu kwa shughuli za uvuvi hivyo, Serikali imejipanga kuwaimarisha kupitia Sekta ya Uchumi wa Buluu kwa kuwapatia Boti za kisasa zenye Mashine na Mitego yenye uwezo mkubwa wa kuvulia Bahari kuu ili kuweza kupata mazao mengi na yenye tija kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.
Amewaahidi kinamama kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Hussen Ali Mwinyi inatekeleza ahadi zake kwa vitendo kwa kuwasaidia kuwawezesha kupitia vikundi vya ushirika ili kujikwamua kiuchumi hivyo, ni busara wakajiunga katika vikundi vilivyosajiliwa kisheria ili kupata kunifaika na mkpo huo.
Amewatoa hofu juu ya changamoto yao ya hospitali na uchavu wa miundombinu ya barabara kwa kuwaahidi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kuzijenga barabara zote kwa kiwango cha Lami sambamba na huduma muhimu za kijamii ikiwemo Hospitali, Skuli na miundombinu ya maji na umeme.
Akitolea ufafanuzi changamoto ya msitu wa ........ambao wananchi wa kijiji cha Kiungoni wamedai msitu huo kuchukuliwa na wananchi wa Kojani Mhe. Hemed amewanasihi wananchi hao kuacha tofauti zao na waishi kwa umoja na ushirikiano wakati ambao Serikali inatafuta ufumbuzi suala la msitu huo.
Amesema Jimbo la Pandani na Kojani lazima yabaki kwa Chama Cha Mapinduzi katika ngazi zote hivyo umoja na msjikamano kwa wana CCM ndizo nguzo pekee za kuipatia usshindi wa kishindo kwa majimbo yote nchini.
Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Wete Ndg. Hamad Omar Bakari ameeleza kuwa Miundombinu ya Mabomba ya Maji Wilayani humo ni chakavu ambapo Serikali inaandaa mradi wa Maji uitwao Zanzibar Water security Project (ZWSP) ambao upo hatua za awali kuanza kwake ambao utamaliza moja kwa moja tatizo la Maji Pandani na maeneo jirani.
Amesema Wizara ya afya inasimamia ahadi ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwajengea Kituo cha Afya kiungoni ambacho tayari mipango ya awali imeshaanza ili kumaliza changamoto inayowakabili wananchi wa eneo hilo kufuata huduma hiyo masafa marefu.
Nae Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Jumuiya ya Wazazi Bi Habiba Ali Muhamed amewasihi vijana kutumia fursa ya elimu bila ya malipo inayotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kupata elimu bora yenye manufaa kwao.
Aidha amemshukuru Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuamua kuwafikia wananchi katika ngazi ya majimbo hatua ambayo inaongeza Imani ya wananchi kwa viongozi wao.
Akipokea wanachama wapya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndg. Hemed Suleiman Abdulla amewataka kushikimana na kukiendeleza Chama na kuwaeleza kuwa CCM ni Chama chenye sera zinazotekelezeka kwa maslahi ya wananchi,
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
28-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
28-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
28-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
28-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
28-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
28-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
28-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
28-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
28-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
28-12-2025