RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AZUNGUMZA NA NA BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA MHE. ELIZABETH JACOBSEN IKULU ZANZIBAR
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya Norway kwa jitihida zake za kuendelea kuiunga mkono Tanznia ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elizabeth Jacobsen aliyefika kuaga baada ya kumaliza kipindi chake cha utumishi nchini.
Rais Dk. Mwinyi alimueleza Balozi Jacobsen kwamba, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi kutoka Norway zikiwemo sekta za Afya, Umeme na Elimu.
Amesema uhusiano wa Norway na Tanzania utakumbukwa zaidi kwa kuinufaisha Zanzibar kupitia sekta ya umeme, hasa wa kutoka Tanga hadi Pemba na Dar es Salaam hadi Zanzibar ambapo Dk. Mwinyi alieleza, Norway ilitoa mchango mkubwa kuunga mkono juhudi za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzaznia katika kuwafikishia huduma bora wananchi.
“Tunaishukuru Serikali ya Norway kwa kuendelea kutuunga mkono Tanzania, hasa kwenye sekta za Afya na umeme, tunashukuru Norway imetuungamkono kwenye sekta ya umeme, ilisaidia kueneza umeme visiwani Zanzibar” alisifu Rais Dk. Mwinyi.
Aidha, Dk. Mwinyi alimueleza balozi huyo dhamira ya Zanzibar kutaka kujitegemea kwa umeme wake wenyewe ili kuwapatia huduma ya uhakika wananchi wa Unguja na Pemba badala ya kutegemea umeme kutoka Tanzania Bara.
“Kwa hatua tuliofikia sasa, Zanzibar inataka isimame wenyewe ijitegemee wenyewe umeme wake utakaozalishwa hapa hapa Zanzibar” alieleza Dk. Mwinyi.
Pia alisifu Rais Dk. Mwinyi, alisifu ushirikiano ulipo baina ya Norway na Tanzania hasa kwenye nyanja za afya na elimu na kueleza Serikali ya Norway imetoa mchango mkubwa kwa Tanzania kwa kuwajengea uwezo Watanzania wengi kupitia vyuo vikuu vya nchi hiyo.
“Hatunabudi kuishukuru Serikali ya Norway, kupitia vyuo vikuu vya afya vya huko vimewajengea uwezo watu wetu kupitia sekta za Umma na binafsi” alisifu Dk. Mwinyi.
Akizungumza na Rais Dk. Mwinyi, Balozi Elizabeth ameisifu Tanzania kuendelea kuwa nchi ya amani, yenye raia wenye upendo, ushirikiano, umoja na utulivu wa kisiasa akieleza kuwa Tanzania ni kielelezo cha nchi ya mfano barani Afrika na kwengineko duniani kuwa ni taifa lenye demokrasia kwa kutekeleza na haki za binaadamu na siasa safi.
Balozi huyo alimuahidi Rais Dk. Mwinyi, kwamba Serikali ya Norway daima itaendelea kuiungamkono Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye sekta za Maendeleo.
Alisema Serikali ya Norway inajivunia uhusiano wa muda mrefu wa diplomasia uliopo baina yake na Tanzania na kusifu zaidi ya miaka 50 yaushirikiano wao kwenye masuala mbalimbali iliwemo ushirikiano walionao baina ya vyuo vikuu vya Norway na Tanzania ni chachu iliyokuza urafiki baina ya watu wa mataifa wawili hayo kwenye nyanja mbalimbali za jamii na uchumi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
25-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
25-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
25-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
25-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
25-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
25-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
25-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
25-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
25-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
25-10-2025