Wazazi na walezi wametakiwa kuwalea watoto wao katika maadili mema ili kupata kizazi chenye hofu ya Allah kitakachosaidia kuziondosha changamoto zilizopo zinazosababishwa na kukosekana kwa maadili mema kwa vijana.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwasalimia waumini wa Masjid JAMII WATHABATUL- KHEIR iliyopo KOANI kwa KOZI Wilaya ya Kati mara baada ya kumaliza Ibada ya Sala ya Ijumaa.
Amesema ni wajibu wa kila mzazi na mlezi kuwalea watoto wao katika maadili mema yatakayowajenga kidini na kiimani jambo ambalo litasaidia Taifa kupata viongozi bora wa baadae na wenye kufanya kazi zao kwa hofu ya Mwenyezi Mungu.
Alhajj Hemed amesema wakati umefika wa jamii kujitathmini katika malezi wanayowalea watoto wao ili kupunguza malalamiko ya mmong’onyoko wa maadili unaopelekea vijana kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo udhalilishaji na utumiaji wa madawa ya kulevya.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed ameendelea kuwasisitiza wananchi wa Zanzibar na Watanzania kwa ujumla kuzidi kudumisha Amani na Utulivu uliopo nchini jambo ambalo huwaweka huru katika kufanya shuhuli zao mbali mbali za kujitafutia maisha kwa faida yao na Taifa kwa ujumla.
Mapema akitoa Khutba katika Sala ya Ijumaa, Sheikh SALIM MASSOUD SEIF amewataka waumini wa Dini ya Kiislam kuendelea kuzilea vyema familia zao ili kuweza kupata watoto wema ambao watakuwa wema sasa na hadi kuondoka kwao duniani.
Amesema kuwa waislamu ni lazima kushirikiana na kuamrishana mambo mema na kukatazana mabaya ili kujikurubisha karibu na Allah (S.W) na kufikia lengo la kuumbwa mwandamu hapa duniani
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
27-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
27-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
27-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
27-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
27-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
27-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
27-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
27-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
27-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
27-10-2025