Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ameutaka uongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) na wanachama wake kuyatumia vyema mafunzo wanayopatiwa ambayo yatawajengea uwezo wa utekelezaji wa majukumu yao ili kuleta mabadiliko ya kiutendaji katika Chama cha Mapinduzi sambamba na kutatua changamoto za wanachama zinapojitokeza
Ameyasema hayo katika ufunguzi wa Semina ya siku moja ya kuwaongezea ujuzi na maarifa Madiwani, Makatibu wa Wadi na Majimbo pamoja wajumbe wa kamati tendaji iliyofanyika katika ukumbi wa Viwanja vya Maonesho Nyamanzi Zanzibar Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.
Mhe. Hemed ameseama moja ya jukumu la UWT ni kutoa elimu kwa wanachama, kuwahamasisha wanawake katika kugombea nafasi za Uongozi, kuishauri Serikali na kutatua changamoto katika jamii kwa lengo la kuweka mustakbali mwema wa Taifa na chama cha Mapinduzi ili kiendelee kushika Dola awamu kwa awamu.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Uongozi ni kuonesha njia kwa wanowaongoza ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na kusema kuwa kufuata maadili ya Uongozi na Utendaji ni jambo la msingi ambalo litasaidia kunyanyua ari kwa wafuasi wa Chama na kuleta maendeleo kwa Jumuiya.
Aidha Mhe. Hemed ametoa wito kwa Viongozi kuzitumia vyema nafasi zao kwa kufuata misingi ya uongozi kwa wanowaongoza ikiwemo nidhamu, uaminifu, uadilifu, unyenyekevu, kujenga umoja, matumizi mazuri ya lugha, kutatua kero na kuandaa viongozi wapya watakaoweza kushika nafasi mbali mbali katika Jumuia.
Sambamba na hayo, Mhe Hemed amesema anatambua kuwa wapo baadhi ya viongozi na watendaji hawana lugha nzuri kwa wanowaongoza hivyo amewataka kujirekebisha na kuachana na tabia hiyo kwani Chama cha Mapinduzi hakitamvumilia mtu yoyote atakae kwenda kinyume na maadili ya Chama, hivyo amewahamasisha wanawake ndani ya Chama Cha Mapinduzi wenye uwezo wa kuongoza kujiandaa na kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi katika Uchagzi Mkuu wa mwaka 2025.
Kwa upende wake Mwenyekiti wa UWT Taifa Bi. Mary Pius Chatanda amezipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kukamilisha vyema na kwa mafanikio makubwa zoezi la sensa la kidigital ambalo halijawahi kutokea nchini ambalo takwimu zake zitalisaidia Taifa katika kupanga mikakati mbali mbali ya kimaendeleo nchini.
Chatanda amewaagiza viongozi ambao wamepatiwa mafunzo hayo kushuka kwa wananchi kusikiliza kero zao zinazowakabili ili kuweza kufanya maamuzi sahihi katika vikao vya chama na Serikali.
Aidha amewataka viongozi wa UWT kuendelea kufanya zoezi la usajili wa wanachama wapya kwa njia ya kielektroniki ambao watasaidia katika kupanga mikakati ya Jumuiya sambamba na kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinashinda kwa kishindo kikubwa katika uchaguzi mkuu wa nchi unaotarajiwa kufanyika mwaka 2025.
Mapema Makamo Mwenyekiti wa UWT Taifa Bi. Zainab Khamis Shomari amesema kuwa Mafunzo hayo waliopatiwa viongozi wa UWT yataleta mabadiliko chanya katika Utendaji kazi wa Jumuiya na Chama kwa Ujumla.
Amesema kuwa UWT wamejipanga kukipigania na kukilinda chama cha Mapinduzi kwa kuhakikisha kinafanya vizuri katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwisho wa mwaka huu na ule uchaguzi Mkuu wa nchi mwaka 2025 CCM inashinda na kuendelea kuiongoza nchi.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
31-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
31-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
31-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
31-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
31-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
31-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
31-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
31-12-2025