Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Ndugu.Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema Chama cha Mapinduzi kinatambua na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na Jumuiya ya wazazi Tanzania katika kuhakikisha CCM inaendelea kushikilia dola awamu kwa awamu
Ameyasema hayo katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla katika uzinduzi wa sherehe za Wiki ya wazazi Kitaifa zinazofanyika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi.
Dkt Mwinyi amesema Jumuiya ya wazazi imekuwa ikifanya kazi nzuri katika kusimamia elimu, maadili na malezi bora kwa watoto yenye kufuata utamaduni wa Kitanzania jambo ambalo linaendelea kuiletea heshima kubwa Tanzania.
Amesema kuwa jumuiya ya wazazi imekuwa mstari wa mbele katika kupiga vita vitendo vya ukatili, unyanyasaji na udhalishaji wa kijinsia jambo ambalo linazorotesha nguvu kazi na maendeleo ya Taifa hivyo ni wajibu wa kila mwanajumuiya kuhakikisha anasimama imara katika kupinga vitendo hivi.
Rais Dkt. Mwinyi amesema mtaji wa chama chochote cha siasa ni wanachama hai hivyo ameitaka Jumuiya ya Wazazi kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na CCM, kuwapa elimu ya kupiga kura pamoja na kuwajenga kuwa na utayari wa kukipigia kura kwa wingi chama cha Mapinduzi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020-2025.
Aidha Makamu Mwenyekiti Mwinyi amewasisitiza viongozi kushuka chini kwa wanachama na kufanya ziara ya kuzitembelea jumuia mbali mbali pamoja na kushika kwa wananchi kusikiliza changamoto zinazowakabili na kuziwasilisha Serikali kupatiwa ufumbuzi kwa maslahi ya chama na serikali.
Rais Dkt Mwinyi amesasisistiza kuwataka Watanzania kuwa Umoja na Mshikamano kwa kuweka mbele maslahi ya CCM hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu ujao ili CCM iendelee kushinda kwa kishindo na kudhikilia madaraka.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa anaefanyia kazi zake Zanzibar Ndugu DOGO IDDI MABROUK amesema Jumiiya ya Wazazi itaendelea kutoa elimu na kuhamasisha juu ya malezi bora ya watoto kwa kutambua tamaduni zao ambazo zinaonekana kutoweka na kusababisha mmong'onyoko wa maadili jambo linalopelekea kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia hasa kwa wanawake na watoto.
Ndugu DOGO amesema kupitia Jumuiya ya wazazi itahakikisha sera tano muhimu za jumuiya hio zinatiliwa mkazo katika utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na elimu, malezi, utamaduni, mazingira na afya ili kuhakikisha CCM inakuwa na wanachama wenye uweledi na wenye kufuata maadili kama sera na miongozi ya chama inavyoongoza.
Akiwasalimia wananchi wa Mkoa wa Katavi Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Mizengo Kayanza Pinda amesisitiza umoja na mshikamano kwa Watanzania wote ambao hujenga upendo miongoni mwao na kupelekea amani na utulivu ambao ndio ngao na muhimili mkubwa wa maendeleo ya Taifa.
Mhe. Pinda amewataka wanakatavi na watanzani wote kuendelea kujiandikisha katika daftari la kupigia kura ili kuweza kupata nafasi ya kukipigia kura kwa wingi chama cha Mapinduzi na kuendelea kukiweka madarakani.
Pinda amesema uhifadhi wa mazingira ni jambo la lazima kwa kila Mtanzania na kuwaomba kuacha tabia ya kukata miti na kuchoma moto kiholela misitu ya hifadhi na badala yake wajenge tabia ya kupanda miti kwa kuhifadhi mazingira.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
25-10-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
25-10-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
25-10-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
25-10-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
25-10-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
25-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
25-10-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
25-10-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
25-10-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
25-10-2025