Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamuwa kujenga Miundombinu ya Barabara ili kurahisisha huduma ya usafiri pamoja na kuongeza kasi ya ukuaji wa Uchumi nchini
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamuwa kujenga Miundombinu ya Barabara ili kurahisisha huduma ya usafiri pamoja na kuongeza kasi ya ukuaji wa Uchumi nchini.
Akiendelea na ziara ya kukagua uhai wa Chama Mkoa wa Kusini Unguja katika Majimbo ya Uzini, Chwaka na Tunguu Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Maamuzi ya Serikali ya Awamu ya Nane inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kujenga Barabara zote za mijini na vijijini kwa Njia ya Lami ni kuwarahisisha wananchi huduma ya usafiri pamoja na kukuza Uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa Ujumla.
Mhe. Hemed amesema wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja wanajishughulisha na kazi za Kilimo na Uvuvi hivyo uwepo wa Barabara hizo kutasaidia mazao ya biashara kufika sokoni kwa wakati yakiwa na kiwango hatua ambayo itarahisisha kuongezeka Uchumi Binafsi na Taifa.
Mhe. Hemed ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Mkoa huo ni sehemu moja wapo yenye shughuli nyingi za kitalii hivyo uwepo wa huduma mbali mbali kutapelekea kwa kiasi kikubwa kuongeza Idadi ya watalii sekta ambayo inasaidia kwa asilimia kubwa kukuza uchumi wa Zanzibar.
Sambamba na hayo Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuendelea kuunga Mkono juhudi za Serikali kwa kutangaza maendeleo yanayofanywa na Viongozi kwa mujibu wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025.
Amesema Serikali zote mbili zinaendelea kuwaletea maendeleo wananchi wake kwa kuzingatia sekta mbali mbali na kueleza kuwa wananchi wana kila sababu ya kuwaunga Mkono Marais wote wawili Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na kuwachagua tena kwa kura nyingi ifikapo mwaka 2025.
Aidha Mhe. Hemed amewapongeza wabunge, Wawakilishi na Madiwani wa Majimbo hayo kwa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi kwa kumsaidia Rais Dkt. Mwinyi majimboni kwa kutatua Changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo hayo.
Nao viongozi wa Majimbo hayo wameeleza faraja yao kwa maamuzi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuelekeza fedha za Mkopo wa kupunguza athari za Uviko 19 kujengea miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Madarasa ambayo yamepunguza uhaba wa eneo la kusomea na kupelekea wanafunzi kuingia kwa mkupuo mmoja kwa siku.
Kwa upande wao wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Mvita Mustafa Ali na Makame Ramadhan Mbanja wamewataka wana CCM kuendelea kuimarisha Chama hicho kwa kusimamia maelekezo yaliyotolewa na Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa maslahi ya chama hicho.
Katika ziara hiyo Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amepokea zaidi ya wanachama wapya Elfu Moja na Mia tatu (1300) kati ya hao wanachama watano (05) kutoka vyama vya upinzani.
Akizungumza kwa niaba yao aliekuwa Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Kati Ndugu. Ali Mbarouk Mshimba ameeleza kuwa ameamua kurudi CCM kutokana na kasi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 inavyotekelezwa na Viongozi wa Chama hicho.
Mapema Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ameshiriki ujenzi wa Tawi la CCM Mgeni Haji na kukagua ujenzi wa Tawi la CCM Kikungwi pamoja na Ukumbi wa Mikutano Chwaka.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
16-12-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
16-12-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
16-12-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
16-12-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
16-12-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
16-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
16-12-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
16-12-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
16-12-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
16-12-2025