AnuaniKisiwandui, Zanzibar
Simu(+255) 26 23 22965

Habari na Matukio Mbalimbali


.DK.HUSSEIN MWINYI ASHUHUDUA ITIAJI WA SAINI YA MRADI WA SEKTA YA AFYA BAINA YA CHINA NA ZANZIBAR IKULU LEO

alternative

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.

Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alikoshuhudia utiaji wa shaini mikataba ya miradi mitano ya ushikirikano kwenye sekta ya afya baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

Katika hafla hiyo Rais Dk. Mwinyi alisema, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi za maendeleo kupitia misaada tofauti inayoletwa kutoka China hasa sekta za Afya na Elimu ikiwemo Tanzania kujifunza uzoefu wa masuala mbalimbali ya afya, kupokea timu za madaktari bingwa wanaofika nchini kwaajili ya kubadilishana uzoefu na wazawa hali aliyoieleza imeimarisha uhusiano mwema uliopo baina yao.

Alisema mikataba minne aliyoishuhudia sio tuu itaimarisha huduma za tiba nchini pekee, lakini itajenga ushirikiano mwema baina ya maofisa wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na China jambo alilolieleza ni ishara ya uhusiano mwema uliopo baina ya mataifa mawili hayo.

Rais Dk. Mwinyi alieleza, uhusiano wa China na Tanzania utakumbukwa zaidi kwa kuinufaisha Zanzibar kupitia sekta ya afya katika suala zima la kuimarisha miundombinu ya afya, vifaa tiba, dawa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa wataalamu wa afya wazawa, pamoja na timu za madaktari bingwa wanaofika Zanzibar kila mwaka kwa nyakati tofauti na Tanzania kwa ujumla, jambo alilolieleza kwamba limeimarisha uhusiano wa China na Tanzania.

Aidha, Dk. Mwinyi alimpongeza Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar, Zhang Zhisheng kwa kazi kubwa anayoifanya ya kukuza ushiriiano uliopo baina ya China na Zanzibar.

 “Wenzetu China mmetusaidia sana hata tukieleza hatutomaliza, nimeshuhudia utiaji wa saini mikataba minne ya ushirikiano baina ya Zanzibar na China, kupitia sekta ya afya, miradi hii itaendelea kuimarisha ushirikiano wetu uliopo” Alisifu Dk. Mwinyi.

Naye, Rais wa taasisi ya Ushirikiano baina ya Afrika na China, (CAPFA) Dk. Li Bin ameeleza miradi hiyo itatatua maradhi sugu jamii hasa kina Mama na kutoa fursa za miradi mbalimbali itakayonufaisha pande zote za ushirikiano wa Nchi hizo na kuboresha huduma za sekta ya Afya.

 

 

 

Dk. Li pia aliisifu Tanzania kwa ukaribu wa kihistoria baina yake na China alioueleza ni wa mda mrefu tokea uhai wa Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere, zaidi ya miaka 50 iliyopita.

Alisema, Tanzania imebarikiwa kuwa na raia wenye ukarimu, upendo na ushirikiano, ambao ni kielelezo chema kwenye kukuza uhusiano uliopo baina yao na China.

Alieleza, ushirikiano huo ni mwendelezo wa fikra njema za waasisi wa mataifa mawili hayo, Mwenyekiti Mao Zedong na Mwl. Julius Kambarage Nyerere na kueleza Serikali ya Jamhuri ya watu wa China inajivunia uhusiano huo kwa maendeleo makubwa yaliyofikiwa na watu wa China na Tanzania ikiwemo kukuza uhusiano wa jamii na uchumi.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Waziri wa Afya, Nassor Mazrui alisema mikataba waliyoisaini mbele ya Rais Dk. Mwinyi itagharimu dola za Marekani 4,76,000 sawa na Shilingi bilioni 1.2 za Tanzania.

Miongo mwa miradi iliyosainiwa ni pamoja na mradi wa Ushirikiano wa hospitali baina ya China na Afrika, Utafiti na udhibiti wa magonjwa ya kitropiki ikiwemo Kichocho, Uchunguzi wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi na kituo cha matibabu ya Mama na Mtoto pamoja na msaada wa vifaa tiba. 

Aidha, hospitali zitakazonufaika na ushirikiano huo ni hospotali kuu, Mnazi Mmoja, Kivunge, Chake chake na Abdallah Mzee Pemba.

alternative alternative alternative
Habari Nyingine
Albamu