Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua mchango mkubwa Unaotolewa na Mashirika ya Umma na itaendelea kuchukua juhudi mbali mbali ili kuhakikisha Mashirika hayo yanafanya kazi kwa ufanisi mkubwa hapa nchini.
Ameyasema hayo katika hafla ya ufungaji wa wiki ya Mashirika ya Umma Zanzibar iliyofayika katika Kiwanja cha Mapinduzi Square Michenzani jijini Zanzibar.
Amesema kwa kutambua umuhimu wa Mashirika ya Umma Serikali imechukua hatua ya kuanzishwa kwa Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar chini ya Sheria Namba 6 ya mwaka 2021 na kupewa jukumu la kuwa msimamizi mkuu na mmiliki pekee wa uwekezaji wa Mashirika ya Umma kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwepo kwa Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar kumechangia kuleta mabadiliko makubwa ya uendeshaji wa Mashirika ya Umma, utoaji wa huduma kwa wananchi na kuchangia kuongezeka kwa kwa mapato ya Serikali ambapo kwa mwaka 2022- 2023 Mashirika ya Umma yameweza kuchangia gawio la Shilingi za Kitanzania Bilioni 13.7.
Mhe.Hemed amesema Shirika la Bandari limeweza kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa meli za mizigo katika bandari ya Malindi kupitia muwekezaji Afrikan Global Logistic(AGL) na kuchochea kuongezeka kwa mapato kutoka shilingi za Kitanzania Bilioni 5.5 hadi kufikia Bilioni 6 kwa mwezi kwa mwaka 2024.
Aidha, Mhe Hemed amefahamisha kuwa Shirika la Bima la Zanzibar limepata mafanikio makubwa kwa kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa wananchi kwa kupitia Mifumo ya Tehama na kuchangia kukua kwa mapato kutoka Bilioni 19 kwa mwaka 2021 na kufikia Bilioni 130.74 kwa mwaka 2024.
Sambamba na hayo amewaagiza viongozi wa Mashirika ya Umma kuendelea kuboresha Mifumo ya utendaji katika utoaji wa huduma ili kuleta ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu na kuendelea kukuza ushirikiano wa karibu kati ya viongozi na Afisi ya msajili wa Hazina kwa kutatua chamgamoto mbali mbali zinapotokezea.
Nae Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe Dkt. Saada Salum Mkuya amesema kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo kwenye Mashirika ya Umma hasa katika kutoa huduma bora kwa wananchi ili kuhakikisha yanakamilisha malengo na mikakati ya Serikali iliyojiwekea.
Dkt. Mkuya amesema azma ya Rais Dkt. Mwinyi ni kuhakikisha kupitia Shirika la Nyumba na Mashirika mengine Zanzibar inakuwa na mji wenye majengo ya kisasa yenye kukidhi huduma zote stahiki ambayo yataufanya Mji wa Zanzibar kuwa wenye haiba na muonekano mzuri utakaoitangaza Zanzibar ndani na nje ya nchi.
Dkt. Saada amewataka wananchi kupuuza uvumi unaotolewa na wasioitakia mema Zanzibar na badala yake kuyatangaza mambo mazuri ya kimaendeleo yanayofanywa na Rais Dkt Hussein Mwinyi kwa Wazanzibari wote.
Kwa upande wake Msajili wa Hazina Zanzibar Bwana WAHIDI MOHAMMED SANYA amesema Afisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar imefanikiwa kuyaunganisha Mashirika 18 ya Umma yaliyopo Zanzibar ambayo yanafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa jambo ambalo linaifanya Afisi ya Msajili wa Hazina kupiga hatua kimaendeleo katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake.
Bwana. WAHIDI amesema Wiki ya Mashirika ya Umma itakuwa endelevu na itafanyika kila mwaka lengo ikiwa ni kuyaweka pamoja Mashirika na kujadili mafanikio lakini pia kutafuta njia muafaka za kupata utatuzi wa changamoto mbali mbali zinazoyakabili mashirika hayo.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametembelea mabanda ya maonesho ya Mashirika ya Umma yaliyojotokeza katika kuadhimisha Wiki ya Mashirika ya Umma Zanzibar iliyofayika katika Kiwanja cha Mapinduzi Square Michenzani jijini Zanzibar.
Mhe Hemed Suleiman amewataka wahudumu wa afya kuwa na bidii na nidhamu kwa wananchi
06-11-2025
SMZ Kuendelea kuweka Mifumo ya Kiteknolojia ya Kisasa
06-11-2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amefanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa SADC
06-11-2025
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Sudan kuimarisha ushirikiano wa uwili na kikanda.
06-11-2025
Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Kikao cha Dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
06-11-2025
CCM KATA YA MWANANYAMALA NA CCM MKOA WA MAGHARIB WATEMBELEA S.G.R DAR ES SAALAM-MOROGORO.
06-11-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, amewataka mabalozi wa mashina ya CCM nchini kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa umakini, ufanisi, na ueledi, kwa kuhakikisha wanachama wote wenye sifa za kupiga kura wanaandikishwa katika zoezi la awamu ya pili la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, linalotarajiwa kufanyika mwezi Februari, mwaka 2025.
06-11-2025
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ambaye Sasa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), jana tarehe 13 Disemba, 2024 jijini Dodoma.
06-11-2025
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa, ametoa uchambuzi wa kina kuhusu ushindi mkubwa wa chama hicho katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Septemba 27, mwaka 2024
06-11-2025
Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM) kimempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi, kwa kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Zanzibar.
06-11-2025